Friday, December 4, 2015

Nini maana ya ulcers?
Ulcers  ama vidonda vya tumbo ni michubuko ama vidonda vinavyotokea kwenye njia ya mfumo wa chakula hasa mfuko wa tumbo (stomach)na sehemu ya awali ya utumbo mwembamba (duodenum).


Ni nini husababisha ulcers?
Kwa kawaida mwili hutengeneza asidi na homoni mbalimbali kwa ajili ya kusaidia mmeng’enyo wa chakula kwenye mfuko wa chakula k.m HCL na Gastric juice. Vimelea hivi vikizidi husababisha michubuko au kudhoofisha kuta za ndani ya tumbo na hivyo kuongeza hatari ya mtu kupata vidonda vya tumbo


 ****Maambukizi ya bakteria aina ya  Helicobacter pylori husababisha mtu aliye kwenye hali hiyo kupata vidonda vya tumbo.****
 

Mwili hujikinga dhidi ya asidi ya tumboni kwa:
Kuruhusu chakula kisafiri kwa spidi inayostahili 
Kutengeneza alkali ili kuleta uwiano na asidi iliyotengenezwa tumboni hivyo chakula kilicho katika utumbo mwembamba huwa hakina asidi wla alkali. 
 Vitu hatarishi vinavyoweza kupelekea vidonda vya tumbo ni nini?
Msongo wa mawazo (stress)
Vinywaji vyenye caffein kama kahawa 
Sigara(nicotine) 
Pombe
Kutokuwa na uwiano sahihi wa kula chakula k.m kula kupitakiasi usiku kwa sababu mchana ulishinda njaa. 
Magonjwa k.m ini 
Kutumia dawa hasa za NSAIDs k.k aspirin 
 Dalili za vidonda vya tumbo
Mara nyingi hutokana na eneo kilipo kidonda
 Mfuko wa tumbo(gastric) 
 - maumivu makali ya tumbo saa1-2 mara baada ya kula
Mwanzo wa utumbo mwembamba (duodenum)
-maumivu makali ya tumbo kabla ya kula (hupungua pale unapokula au maziwa)
-maumivu makali ya tumbo usiku wa manane
Dalili za jumla
-kupungukiwa na damu mwilini
-choo kuwa na rangi nyeusi(melena) 
 -kutapika damu (haematemesis)

  -kukosa hamu ya kula

  -kuwa na kiungulia

  -maumivu ya kifua


Dalili za hospitali
-kuuma tumbo akiguswa 
 -tumbo kuunguruma (succission splash) 
- H pylori wakiotesha damu 
 Madhara ya vidonda vya tumbo
Kwa watoto ni utapiamlo

Kutoboka kwa utumbo

Maambukizi ya bakteria wengine kupitia katika kidonda

Kupungukiwa damu

Kupungukiwa uzito

Vidonda kupeleka magonjwa mengine kama gastric outlet obstruction(GOO)
Matibabu 
Matibababu ya madawa ya hospitali  
  mgonjwa hupewa dawa hospitali za kupunguza asidi na kuua bacteria wa H pylori. Kidonda hubaki kwa muda mrefu k.m omeprazole, flagyl na amoxicilin kwa walau wiki mbili.
Matibabu ya upasuaji hospitali 
Hii ni kwa baadhi ya wagonjwa ambao vidonda vyao ni sugu, vikubwa vyenye hatari ya kutoboa 
utumbo 
 Matibabu asilia ya vidonda vya tumbo
       •Matibabu asilia ya vidonda vya tumbo inahusisha virutubisho mbalimbali muhimu kwa ajili ya kuleta uwiano wa asidi mwilini, kuua bakteria wa H pylori na kuponya vidonda vyenyewe pamoja na mabadiliko kwa mtazamo wa maisha bora zaidi.
 Mgonjwa wa vidonda vya tumbo afanye yafuatayo:
Kunywa maji safi na salama lita 2-3 
Kupunguza matumizi ya kahawa yenye caffeine 
Kuepuka kula mlo mmoja mwingi baada ya kukosa mingine k.m usiku 
Epuka vyakula vinavyokuletea aleji 
Asinywe pombe 
Kutotumia dawa kama za NSAIDs kama aspirini
Asivute sigara 
Ale chakula kwa wastani kwa vipindi 
Asitumie dawa za NSAIDs kama aspirini 
Atumie virutubisho muhimu vya asilia kwa ajili ya ugonjwa 
wake wa vidonda vya tumbo
 Virutubisho muhimu kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo
Mgonjwa wa vidonda vya tumbo anakabiliwa na: 
  - maambukizi ya bakteria wa H pylori 
  - kuta dhaifu za tumbo 
  - vidonda katika tumbo
- upungufu wa damu 
 PATA VIRUTUBISHO MUHIMU KWA AJILI YA TATIZO HILO
PHONE: =+255717962720
               = +255767962720

0 comments:

Post a Comment

Mr.Mputa

You are welcome in this blog you ca get us through..
Mobile+255717962720
+255767962720
Njombe Iringa Tanzania

TANGAZO

Karibuni katika Blog ya Jiliwaze hapa utapata mambo mbali mbali yakufunza na kuonya na kama unahitaji kutengenezewa email,facebook ac,page ama blog wasiliana nasi kupitia.. Phone:0717962720/0767962720 Email:mputae@yahoo.com :mputae@rocketmail.com

Popular Posts