UNAHISI
mwenzi wako anakusaliti kwa maana kwamba anafanya ngono na wanawake au
wanaume wengine? Fahamu kuwa wapo wengi wenye kulalamikia hilo.
Kuna
baadhi ya watu wamekuwa wakijiuliza kwanini hasa anatoka na wengine
ikiwa aliahidi kwamba atakuwa ananipenda milele? Wengine wanakwenda
mbali zaidi na kufikiri kila kitu ambacho anakifanya kwa mwenzi wake
kitakuwa ni chenye kumpendeza mwingine.
“Mimi najitahidi kumfanyia mambo mengi mazuri, bado anaonekana haridhiki,” ndivyo baadhi ya watu wanavyojisemea.
UKWELI UKOJE?: Ni vizuri katika mapenzi kupata muda wa kuzungumza
mwenzangu unapendelea nini na usingependa ufanyiwe nini.KUAMINI KUWA
UNAYOFANYA NI MAZURI, BILA KUAMBIWA NA UNAYEMFANYIA, SIO SAHIHI.
Maisha ya raha katika uhusiano ni kuhakikisha kunakuwa na fursa ya
wapendanao kukaa na kujadili namna gani wamekuwa wakiishi na nini cha
kufanya ili waweze kuwa na maisha bora zaidi.
KUKWAZANA NI MAMBO YA
KAWAIDA KATIKA MAPENZI. IKIWA UMEKAA KWENYE TUMBO LA MAMA YAKO NA BADO
KUNA WAKATI MNAKWAZANA, IWE MTU AMBAYE MMEKUTANA TU MITAANI?Jambo muhimu
katika ndoa ni kuhakikisha kunakuwa na nafasi ya wanandoa kujadili hali
ya ndoa yao.
Kama ilivyo katika biashara kwamba wafanyabiashara
wakati fulani wanajadili hali ya maendeleo ya biashara ili kujua kama
kuna matatizo gani nk, ni muhimu sana wanandoa kutenga muda wa kujadili
hali ya uhusiano wao.
SABABU ZA WATU KUSALITIWakati fulani nimekuwa
nikiongea na watu wanaosaliti ndoa...baadhi yao ukiwauliza unaonaje sasa
ukaondoa kwenye ndoa na kuoana na huyo wa nje, jibu ni kwamba hawezi
kwa sababu anasaliti si kwa sababu hampendi aliyenaye, bali wakati
mwingine ni kutofautiana.
Kwa mfano katika utafiti wangu nimegundua
kwamba idadi kubwa ya wanandoa waume, hawana uhakika wa kupata tendo la
ndoa kwa wakati wanaotaka, kama ilivyo kwa baadhi ya wanawake.
Tafiti ambazo nimekuwa nikifanya pia nimegundua kuna tofauti ya mahitaji
katika ndoa, kwa mfano wakati wanaume ni wenye kuhitaji mno tendo la
ndoa, furaha ya wanawake walio wengi sio hilo wakati fulani ni uhakika
wa kupatikana kwa mahitaji ya ndani na amani.
*Kutopata mapenzi ya
kweli katika ndoa hasa ikiwa Kijana/Binti alilazimishwa kuoa/kuolewa na
mtu ambaye hakumpenda.-Wengine hawapata mapenzi ya kweli kwa sababu tu
mwanaume au mwanamke hamjali, kitendo ambacho kinasababisha baadhi yao
kuona kwamba suluhu pekee ni kwenda nje ya ndoa.
*Uchafu, kutojijali
au kujipenda kwa mwanaume na mwanamke-Wapo wanaume na wanawake ambao
wamekuwa wachafu wa mwili na kutojipenda, kiasi kwamba ukiwa nae unahisi
kichefuchefu. Kuna wanaume na wanawake kwa mfano wanalala bila kuoga,
wengine unakuta mwingine mlevi, mwingine hanywi, kisha anarudi nyumbani
anaomba abusiwe...mhh! raha iko wapi hapa?*Kutotosheka/kuridhika katika
tendo la ndoa
-Ingawa wakati mwingine huwa ni uroho wa mtu, mara
nyingi hata majumbani watoto kama hawajashiba, baadhi yao hukimbilia
kudowea chakula kwa jirani.
*Ubize wa kazi kupita kiasi/Kusafiri
-Kuna watu wako bize kila kukicha, wakati mwingine si kweli kwamba wako
bize bali ni unafiki au labda kutojua namna ya kupangilia mambo. Wengine
ni watu wa safari kila mara, hiyo ni mbaya kwa wanandoa.
*Tamaa ya
mali: Kuna wengine wako tayari kufanya ngono hovyo ili wapate mali. Huu
ni ujinga, badala ya mtu kufanya kazi, anafikiri kwamba njia rahisi ni
kubabaikia wanaume wenye magari, wenye fedha nk.
*Kujifunza mambo au
mitindo mipya -Wakati mwingine kuna wengine wanatoka nje ili kusaka
miondoka mipya...kuna wengine wamekuwa waoga wa kusema ukweli kwa wenzi
wao juu ya yale ambayo wanayataka, matokeo yake wanaona wafanye hiyo
‘dawa mbadala’.
*Kutopata tendo la ndoa muda mrefu, labda kwa sababu
mume ana matatizo au mke ana uja uzito mkubwa ama amejifungua n.k-Hata
hivyo kitaalam kuna njia za kuridhishana si lazima tendo la ndoa la aina
moja, bali wapenzi wanaweza kuchezeana na kila kitu kikawa chenye
kuwafurahisha wote au kumfanya mwenzi wake afurahie.
Sunday, September 1, 2013
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment