Thursday, November 12, 2015


(1). Kuchagua Kazi.
Ni vigumu kupata Kazi ukiwa nje ya Kazi. Fanya Kazi uliyoipata upate Kazi unayoitaka.
(2). Kuchagua sehemu ya kuishi /kufanyia Kazi.
Maisha ni safari ndefu, maisha ni popote, si lazima kukaa mjini. Hauwezi kujua ni sehemu gan iliyobeba mafanikio yako. Chagua sehemu yenye FURSA na si yenye  MAGHOROFA.
(3). Kuishi bila kuwa na malengo.
Maisha si bahat mbaya au nzuri. Maisha ni mipango, Maisha yanaongozwa na malengo. Vile ulivyo leo ni matokeo ya jinsi  ulivyopanga jana, na vile unavyoishi leo ndivyo kesho yako itakavyokuwa. PANGA KESHO YAKO SASA.
(4). Maisha Ya kuiga.
Maisha yako si ya mwenzako, na ya maisha ya mwenzako si ya kwako. Si kila ukionacho ni lazima ufanye, chagua kipi cha kufanya na kipi cha kuacha. Kupitwa na jambo wakat mwingine sio USHAMBA ni BUSARA.
(5). Kuishi juu ya kipato chako.
Ishi kulingana na vile ulivyonavyo na si usivyonavyo. Kuwa na Busara katika MATUMIZI uepukane na MADENI yasiyo na ULAZIMA. RIDHIKA NA VILE ULIVYONAVYO.
(6).Kuishi bila AKIBA.
kuweka akiba ni TABIA sio kiwango kikubwa cha Pesa. Jenga tabia ya kujiwekea akiba. Haujui ni kipi kitakupata muda USIOTEGEMEA.
(7). Kuishi kwa kutegemea MSHAHARA.
Mshahara haujawahi kutosha na hautatosha kama ukishindwa kuishi chini ya kipato chako  na kuwa na njia mbadala za kuinua kipato chako. JARIBU NJIA ZINGINE MBALI NA MSHAHARA.
(8).Kushindwa Kupangilia MATUMIZI ya Pesa.
Maamuzi yako ya pesa ndiyo yatajayoamua hali yako ya kiuchumi baadaye. Ni muhimu kujua kipi cha kununua, kwa wakat gani na kwa sababu gani. Jifunze kutofautisha kati ya liability (dhima) mfano: gari ya kutembelea na assets (kitegauchumi) mfano:nyumba au kiwanja . TUMIA PESA YAKO KUNUNUA ASSETS KULIKO LIABILITY.
(9).Kushindwa kutumia MUDA wako VIZURI.
Changamoto kubwa inayotukabili vijana ni kushindwa kujua namna ya kutumia vizuri muda. Tumia muda wako mwingi kujiendeleza ufahamu wako kwa kujisomea, kupanga malengo yako ya maisha, kujiuliza ni wapi ulikosea na nini ufanye ili urekebishe hayo makosa na muda mchache ufanye wa mapumziko na kufanya vitu vya kufurahisha akili yako kama kuangalia movie, mpira, kuingia kwenye mitandao ya kijamii Facebook, watsap n. k. Kumbuka muda ni rasilimali isiyoweza kurudishwa pindi unapopotea.
(10).Kuaoa bila ya kujipanga kimaisha. (premature marriage).
Hii inawahusu wanaume, swala la kuoa ni pana sana na kila mtu ana vigezo vyake na mtazamo wake kufanikisha jambo hilo. Ila jambo la msingi ni hili, jiandae kwanza kiuchumi kabla hujaingiza majukumu mengine, unapoa ujue umekubali kusaidia upande wa mwanamke, upande wa familia yenu bila kusahau familia yako binafsi. Hata kama maisha ni kusaidiana na huyo utakayemuoa ila nafas yako kama mwanaume ITABAKI pale Pale. JIPANGE KWANZA.
MWISHO : UJANA NI KIPINDI AMBACHO NAKIFANANISHA NA KAMA SHAMBA LENYE UDONGO MZURI LINALOPOKEA KILA AINA YA MBEGU.. SASA ITATEGEMEA UNAPANDA NINI..!
*****Panda Chema Uvune Mema ***
JITAMBUE SASA.......! 
KWA ELIMU ZAIDI Piga: +255767962720
                               or : +255717962720

0 comments:

Post a Comment

Mr.Mputa

You are welcome in this blog you ca get us through..
Mobile+255717962720
+255767962720
Njombe Iringa Tanzania

TANGAZO

Karibuni katika Blog ya Jiliwaze hapa utapata mambo mbali mbali yakufunza na kuonya na kama unahitaji kutengenezewa email,facebook ac,page ama blog wasiliana nasi kupitia.. Phone:0717962720/0767962720 Email:mputae@yahoo.com :mputae@rocketmail.com

Popular Posts