Tuesday, September 6, 2016


Kamsemo ambako kalikuwa kananitia moyo na kuendelea kufikiria ajira tu peke yake wakati maisha hayabadiliki ni haka "maisha hayana formula banah" kiukweli msemo huu ulikuwa unanifanya nijione kuwa ipo siku nitafanikiwa kwa miujiza, lakini muda fulani nilikuwa naona haina haja kujihangaisha kwasababu nimeshaambiwa maisha hayana formula(kanuni) sasa kilichonistua ni kuwa umri unakwenda miaka inapita nikaanza kustuka nikaanza kujiuliza kama maisha hayana kanuni mbona vijana wenzangu wanabadilisha maisha yao wakati mimi niko hapa hapa, mbona Kuna vijana kama mimi wanavipaji vyao na hawahangaishwi na ajira hahahaaaa nikagundua nimebeba mzigo kichwani kwangu kale kausemi kuwa maisha hayana formula, usemi huu umewafanya vijana wengi sana na hata ambao sio vijana kusema ipo siku nitafanikiwa tu halafu kulala ndani.
Usemi huu umewafanya vijana wengi kuendelea kukaa vijiweni wakipiga story wakitiana moyo kizembe eti ipo siku maisha yatakuwa mazuri wakati wapo kijiweni, usemi huu umewajaza nyumbani vijana ambao wamemaliza Chuo wakiamini ipo siku watapata ajira tu kwasababu maisha hayana kanuni wamesahau kujiajiri, hakuna mafanikio ya bahati mbaya, kama na wewe bado umekariri maisha hayana kanuni leo nakwambia futa huo usemi kichwani Kwako maisha yana kanuni zake ambazo kama kweli unataka kufanikiwa lazima ukubali kuzifata kama hauko tayali utaendelea kuwa mkia siku zote za maisha yako.
KUSEMA MAISHA HAYANA KANUNI NI UVIVU WA KUFIKIRIA
,

Kanuni ya kufanikiwa kuwa mjasiriamali ni kuanza kuhudhuria mafunzo na semina mbalimbali za ujasiriamali usipofanya hivyo utasikia mafanikio kwa jirani watu ninaowafundisha kutoka kwenye ajira hadi kujiajiri nawaambiaga hili,sasa usidhani utapata mafunzo haya bure, kama hauko tayali kulipia gharama za mafanikio yako endelea kusema maisha hayana formula, kanuni ya kufanikiwa katika sehem uliopo ni kutenda bila kuogopa na kukata tamaa, sasa unamkuta mtu kaonyeshwa fursa unamsikia nitafanya kesho, endelea kuahirisha tu, mwingine ameingia kuanzisha kitu siku mbili anataka kufanikiwa, asipofata kanuni ya uvumilivu na kutokukata tamaa hata kama atashindwa mara ngapi halafu anataka maisha mazuri imekula Kwake. Maisha yanakanuni zake ukizifuata utafanikiwa, endelea kufatulia makala hizi siku moja tafundisha.
USIPOKUWA TAYALI KUZITAFUTA NA KUZIFATA KANUNI ZA MAISHA, MAISHA MAZURI UTAYASIKIA KWA JIRANI
USIKATE TAMAAA KATIKA MAISHA
 
*** JITAMBUE **

The right action = Success
Nicheki whatsapp -
0767962720 / 0717962720

0 comments:

Post a Comment

Mr.Mputa

You are welcome in this blog you ca get us through..
Mobile+255717962720
+255767962720
Njombe Iringa Tanzania

TANGAZO

Karibuni katika Blog ya Jiliwaze hapa utapata mambo mbali mbali yakufunza na kuonya na kama unahitaji kutengenezewa email,facebook ac,page ama blog wasiliana nasi kupitia.. Phone:0717962720/0767962720 Email:mputae@yahoo.com :mputae@rocketmail.com

Popular Posts