Posted by GLOBAL on February 18, 2012 at 7:00am
4 Comments
0 Likes
Na Shakoor Jongo
MLIMBWENDEanayeshikilia taji la Miss Kinondoni, Stella Mbuge juzikati alivamiwa na vibaka maeneo ya Mwenge jijini Dar na kuporwa simu ya mkononi na fedha.
Tukio hilo lilimkuta mrembo huyo alipokuwa akitembea kwa miguu mida ya saa saba mchana akielekea nyumbani kwao Mwenge jijini Dar.
Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo, Mbuge alikuwa akitembea kwa miguu huku akiwasiliana na mtu mwingine kwa kutumia simu yake aina ya Nokia yenye thamani ya shilingi laki mbili.
“Ghafla walitokea vibaka ambapo mmoja alimpiga kofi kwenye sikio…
Na Shakoor Jongo
MLIMBWENDEanayeshikilia taji la Miss Kinondoni, Stella Mbuge juzikati alivamiwa na vibaka maeneo ya Mwenge jijini Dar na kuporwa simu ya mkononi na fedha.
Tukio hilo lilimkuta mrembo huyo alipokuwa akitembea kwa miguu mida ya saa saba mchana akielekea nyumbani kwao Mwenge jijini Dar.
Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo, Mbuge alikuwa akitembea kwa miguu huku akiwasiliana na mtu mwingine kwa kutumia simu yake aina ya Nokia yenye thamani ya shilingi laki mbili.
“Ghafla walitokea vibaka ambapo mmoja alimpiga kofi kwenye sikio alilokuwa akizungumza na simu na wengine wakafanya kazi ya kumpora simu na kukimbia,” kilisema chanzo chetu.
Alipotafutwa Mbuge alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa hakuporwa simu pekee bali na fedha kiasi cha shilingi 150,000.
“Ni kweli nimeibiwa simu, lakini hata fedha zangu laki moja na nusu pia walizichukua,” alisema.
0 comments:
Post a Comment