Sunday, February 19, 2012

Zimbabwe yaondolewa vikwazo na EU

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe

Muungano wa Ulaya umewaondolea vikwazo baadhi ya maafisa wakuu wa serikali ya Zimbabwe, ingawa utaendelea kushikilia mali ya rais wa nchi hiyo Robert Mugabe pamoja na washirika wake wa karibu.
Kwa mujibu wa muungano huo, vikwazo vya usafiri dhidi ya mawaziri wawili viliondolewa ili kushinikiza serikali kuharakisha mchakato wa mageuzi.

Lakini msemaji wa chama cha rais Robert Mugabe,alipinga hatua hiyo akitaja vikwazo hivyo kama vinavyokiuka sheria, vyenye misingi ya ubaguzi wa rangi na vitakavyoathiri uchumi wa nchi.
Muungano huo pia uliondoa takriban kampuni ishirini za serikali kwenye orodha hiyo ambazo muungano huo ulidai kuwa zilisaidia kufadhili vurugu nchini Zimbabwe.

Ingawa Zimbabwe imepiga hatua katika mchakato wa kuunda katiba mpya, na kuimarisha uchumi, Muungano huo ungali na wasiwasi ikiwa ahadi zilizowekwa baada ya uchaguzi uliokumbwa na vurugu mwaka 2008, ikiwemo ahadi za kufanyia mabadiliko idara ya polisi hazijaweza kutimizwa.

0 comments:

Post a Comment

Mr.Mputa

You are welcome in this blog you ca get us through..
Mobile+255717962720
+255767962720
Njombe Iringa Tanzania

TANGAZO

Karibuni katika Blog ya Jiliwaze hapa utapata mambo mbali mbali yakufunza na kuonya na kama unahitaji kutengenezewa email,facebook ac,page ama blog wasiliana nasi kupitia.. Phone:0717962720/0767962720 Email:mputae@yahoo.com :mputae@rocketmail.com

Popular Posts